Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wajumbe wamtibua mwenyekiti wa CCM Katavi
Habari za Siasa

Wajumbe wamtibua mwenyekiti wa CCM Katavi

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana
Spread the love

MWENYEKITI wa CCM wa Mkoa wa Katavi anayemaliza muda wake mwaka huu, Mselemu Abdallah ameandika barua ya kujiondoa dakika za mwisho madai kuwa ametofautiana wajumbe wa halmashauri Kuu ya CCM mkoa huo, anaandika Mwandishi Wetu.

Akizungumza na wajumbe, Mselemu alikiri kuandika barua ya kujiondoa kugombea nafasi hiyo na tayari ameishakabidhi kwa Katibu wa CCM wa mkoa wa Katavi.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya kikao cha halmashauri kuu ya CCM, kilichofanyika wiki iliyopita katika ukumbi wa CCM wilaya ya Mpanda, kada huyo kajiondoa baada ya kutofauatina na wajumbe wa kikao.

Inadaiwa kuwa siku hiyo kikao hicho kilichokuwa kikiongozwa na yeye kilikuwa kinawajadili na kuwapitisha majina ya wana CCM waliokuwa wakiomba kuteuliwa kugombea nafasi mbalimbali.

Mwenyekiti huyo alikuwa hataki baadhi ya wagombea majina yao yapitishwe na kikao hicho wakiwemo baadhi ya viongozi wa sasa wanaotoka kwenye baadhi ya kata na wengine ambao yeye alikuwa amewasimisha uongozi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!