Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu aibwaga serikali, apata dhamana
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu aibwaga serikali, apata dhamana

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Singida (katikati), akiinga ndani ya chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu
Spread the love

TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, hatimaye amepata dhamana baada ya ombi la mawakili wa serikali la kuomba mahakam imnyime dhamana kutupiliwa mbali, anaandika Hellen Sisya.

Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri amesema, baada ya kupitia hoja za serikali na majibu ya mawakili wa utetezi, haoni mantiki ya kuzuia dhamana kwa Lissu.

Hivyo, Hakimu Mashauri amemtaka Lissu kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambapo kila mmoja atasaini bondi ya Sh. 10 milioni.

Lissu ametimiza masharti hayo na kuachiwa kwa dhamana, lakini anatakiwa kupewa kibali cha mahakama kila anapotaka kutoka nje ya Dar es Salaam.

Kesi itasikilizwa Agosti 24, 2017 na upande wa serikali imesema upepelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Baada ya kuachiwa Lissu na mawakili wake wamezuiwa kuzungumza nje ya mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!