Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakili Makene alilia fedha za ada ya TLS
Habari Mchanganyiko

Wakili Makene alilia fedha za ada ya TLS

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

WAKILI wa kujitegemea ambaye pia ni mwanachama wa Chama Cha Mawakili Tanzania Bara(TLS), Emmanuel Makene amekilalamikia Chama hicho kuwa hakiwasaidii wanachama wake wakati wanatoa ada kila mwaka, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makene, amesema kila mwaka mwanachama analipa zaidi ya Tsh. 2,000,000 kwenye chama cha Mawakili lakini pesa hizo haziwasaidii kwa chochote kwani hata wakipata tatizo hakuna msaada wowote kutoka katika chama hicho.

“Wawakili tunatumia zaidi ya 2,000,000 hadi 4, 000,000 kwa mwaka kwa kulipa kwenye chama cha mawakili,” anasema Makene.

Amesesma kuwa kwa mawakili wapya hali hiyo inawawia vigumu kwani kabla msomi huyo hajasajiliwa anatakiwa kulipa pesa kwenye chama bila hivyo hawezi kupewa usajili.

“Kwa mawakili wapya kabla mtu hajasajiriwa kuwa wakili anapaswa alipe hela kwenye chama. Sasa kwa mtu anayemaliza chuo anapata wapi hela za kulipa?” anahoji Makene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!