Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Bodi mpya NCAA yaahidi kutatua changamoto
Habari Mchanganyiko

Bodi mpya NCAA yaahidi kutatua changamoto

Kaimu Mwenyekiti mpya wa bodi ya NCAA, Mudhihir Mudhihir
Spread the love

BODI ya Mamlaka ya Ngorongoro (NCAA), imesema itakabiliana na changamoto zinazoikabili mamlaka hiyo kufikia dira ya uhifadhi, anaandika Mwandishi Wetu.

Kaimu Mwenyekiti mpya wa bodi hiyo, Mudhihir Mudhihir, amesema hayo juzi baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe kuizindua jijini hapa.

Amesema wajumbe wa bodi hiyo ambao ni wabobezi wa taaluma mbalimbali na uzoefu wataweza kuisimimia mamlaka hiyo kufikia azma yake.

“Kila mmoja wetu hapa ana taaluma aliyobobea nayo, kwa mfano, tunao wataalam wa IT, wastaafu wa jeshi na wanasiasa…na muunganiko huo utaweza kuleta matunda mazuri kwa mamlaka,” amesema.

Wajumbe wa bodi mpya, imechukua nafasi ya bodi ya zamani ambayo muda wake ulimalizika Mei mwaka huu.

Wajumbe wa bodi ya sasa ni Simon Sayore, Brigadia Jenerali mstaafu Aloyce Mwanjile, Dk. Aikande Kwayu, Godfrey Leyla na Mhandisi Peter Ulanga.

Wengine ni Profesa Audax Mabula, Dk Fred Manongi, Profesa Kalunde Sibuga na mbunge wa zamani wa Namtumbo, Vita Kawawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!