Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Wakili Makene alilia fedha za ada ya TLS
Habari Mchanganyiko

Wakili Makene alilia fedha za ada ya TLS

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

WAKILI wa kujitegemea ambaye pia ni mwanachama wa Chama Cha Mawakili Tanzania Bara(TLS), Emmanuel Makene amekilalamikia Chama hicho kuwa hakiwasaidii wanachama wake wakati wanatoa ada kila mwaka, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makene, amesema kila mwaka mwanachama analipa zaidi ya Tsh. 2,000,000 kwenye chama cha Mawakili lakini pesa hizo haziwasaidii kwa chochote kwani hata wakipata tatizo hakuna msaada wowote kutoka katika chama hicho.

“Wawakili tunatumia zaidi ya 2,000,000 hadi 4, 000,000 kwa mwaka kwa kulipa kwenye chama cha mawakili,” anasema Makene.

Amesesma kuwa kwa mawakili wapya hali hiyo inawawia vigumu kwani kabla msomi huyo hajasajiliwa anatakiwa kulipa pesa kwenye chama bila hivyo hawezi kupewa usajili.

“Kwa mawakili wapya kabla mtu hajasajiriwa kuwa wakili anapaswa alipe hela kwenye chama. Sasa kwa mtu anayemaliza chuo anapata wapi hela za kulipa?” anahoji Makene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!