Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakili Makene alilia fedha za ada ya TLS
Habari Mchanganyiko

Wakili Makene alilia fedha za ada ya TLS

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

WAKILI wa kujitegemea ambaye pia ni mwanachama wa Chama Cha Mawakili Tanzania Bara(TLS), Emmanuel Makene amekilalamikia Chama hicho kuwa hakiwasaidii wanachama wake wakati wanatoa ada kila mwaka, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makene, amesema kila mwaka mwanachama analipa zaidi ya Tsh. 2,000,000 kwenye chama cha Mawakili lakini pesa hizo haziwasaidii kwa chochote kwani hata wakipata tatizo hakuna msaada wowote kutoka katika chama hicho.

“Wawakili tunatumia zaidi ya 2,000,000 hadi 4, 000,000 kwa mwaka kwa kulipa kwenye chama cha mawakili,” anasema Makene.

Amesesma kuwa kwa mawakili wapya hali hiyo inawawia vigumu kwani kabla msomi huyo hajasajiliwa anatakiwa kulipa pesa kwenye chama bila hivyo hawezi kupewa usajili.

“Kwa mawakili wapya kabla mtu hajasajiriwa kuwa wakili anapaswa alipe hela kwenye chama. Sasa kwa mtu anayemaliza chuo anapata wapi hela za kulipa?” anahoji Makene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!