Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Vyuo vikuu vya ‘wababaishaji’ kukiona
Elimu

Vyuo vikuu vya ‘wababaishaji’ kukiona

Spread the love

TUME ya vyuo vikuu nchini (TCU), imesema itachukua hatua kali za kisheria dhidi ya vyuo vikuu ambavyo vitatangaza kozi ambazo hazitambuliki na tume hiyo pamoja na Baraza la Taifa la Elimu ya ufundi (NACTE), anaandika Hellen Sisya.

Akizungumza na wanahabari, Eleuther Mwageni, Kaimu Mkurugenzi wa TCU amevitaka baadhi ya vyuo ambavyo tayari vimeonekana kutangaza kozi zisizotambulika na tume hiyo kuacha mara moja, kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

“Wakiendelea kufanya hivyo, tunafata sheria zetu, tutachukua hatua stahiki ……..kuna adhabu zinatolewa,” amesema Mwageni.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi huyo amewataka waombaji wa nafasi za masomo ya elimu ya juu nchini kuomba kozi ambazo zinatambulika na tume hiyo pamoja na NACTE na kuvisisitiza vyuo vikuu kote nchini kudahili wanafunzi wenye sifa na vigezo stahiki katika kila kozi.

Zoezi la uombaji wa vyuo kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu hapa nchini linatarajia kuanza tarehe 22 Julai, mwaka huu ambapo wahitimu wa elimu ya kidato cha sita pamoja na wahitimu wa ngazi ya stashahada wenye sifa stahiki wataomba kudahiliwa na vyuo vikuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!