Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bonde la Wami Ruvu kutangazwa hifadhi
Habari Mchanganyiko

Bonde la Wami Ruvu kutangazwa hifadhi

Mto wa Mfizigo ulioko Matombo Morogoro ambao unakuja kuungana na Mto Ruvu
Spread the love

WIZARA ya Maji na Umwagiliaji kupitia Bonde la Wami Ruvu inakusudia kutangaza  eneo hilo kama  hifadhi ya vyanzo vikuu vya maji nchini, anaandika Christina Haule.

Endapo eneo hilo litatangazwa kama hifadhi kutasaidia kulinda na kutunza mazingizra ili liendelee kutoa maji ya uhakika.

Ofisa kutoka Bonde hilo, Grace Chitanda amesema hayo leo hii wakati akiongea na waandishi wa habari na kwamba uhifadhi huo tayari wameshaanza katika eneo la Makotopola  mkoani Dodoma na wanatarajia kuendelea katika maeneo mengine.

Amesema uhifadhi huo wa vyanzo vya maji  utasaidia kurejesha hali ya uoto wa asili katika vyanzo hivyo na hivyo kuwa kivutio.

Aidha amesema kwa mkoa wa Morogoro wanatarajia kutangaza kuwa hifadhi katika Bwawa na la Mindu na maeneo mengine oevu yenye vyanzo vikuu vya maji.

Ameongeza kuwa shughuli za kibinadamu zinazofanywa kwenye vyanzo vya maji mara nyingi zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa kuharibu na hatimaye hata kukausha vyanzo vya maji na hivyo uhifhadhi huo utasaidia kuleta maana.

Hata hivyo amesema kabla ya kuchukua uamuzi wa kufanya hifadhi wanatekeleza sheria zilizopo za uhifadhi wa maji ili kuweza kuwakamata watakaohusika na uharibifu wa vyanzo vya maji.

“Kwa mfano mtu akifanya shughuli zozote za kibinadamu jirani na vyanzo vya mji ndani ya mita 60 kuanzia chanzo cha maji atafungwa ama atalipa faini isiyopungua Sh. milioni 10,” amesema Chitanda.

Naye Mkuu wa Maabara ya maji mkoani Morogoro, Peter Mhina, amesema uhifadhi huo unapaswa kufuatwa ili kulinda watumiaji na viumbe hai visiweze kupata madhara yoyote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!