VICENT Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema, wabunge wawili na viongozi wengine waliokamatwa juzi na Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma leo wameachiwa, anaandika Mwandishi wetu.
Taarifa za kuachiwa huru kwa viongozi hao imetolewa na Tumaini Makene, Afisa Habari wa Chama hicho ambapo waliokamatwa ni pamoja na Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na Mbunge wa Viti Maalumu, Zubeda Sakuru kwa kile kilichoelezwa kuwa ni maagizo aliyopewa ODC wa Nyasa kuwakamata na kuwaweka selo kwa saa 48.
Wengine waliokuwa wamekamatwa ni Philbert Ngatunga (Katibu wa Kanda), Ireneus Ngwatura (M/kiti Mkoa), Delphin Gazia (Katibu Mkoa), Asia Mohamed (Afisa Kanda), Cuthbert Ngwata (M/kiti Wilaya), Charles Makunguru (Mwenezi Wilaya).
Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chama hicho amesema “Tumepata taarifa viongozi wentu akiwemo Katibu Mkuu wetu na kuwa kesho wanatakiwa kutipoti, sasa haieleweki ni kwa RPC au ni kwa Mkuu wa Mkoa au kwa mkubwa gani mwengine lakini tumeambiwa kuwa anatakiwa kutipoti mahali.
“Hivi tunavyozungumza utaratibu unafanywa kwa taarifa ambazo sina sababu ya kuzitilia shaka Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu kufikishwa Mahakamani na kushitakiwa kwa kosa kwa kosa la uchochezi”.
Lissu amesema, kuna wanachama wa Chadema zaidi ya 51 Wilayani Chato ambao walidiliki kuifanya mkutano wa ndani.
Leave a comment