Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Vongozi Chadema waachiwa
Habari za Siasa

Vongozi Chadema waachiwa

Spread the love

VICENT Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema, wabunge wawili na viongozi wengine waliokamatwa juzi na Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma leo wameachiwa, anaandika Mwandishi wetu.

Taarifa za kuachiwa huru kwa viongozi hao imetolewa na Tumaini Makene, Afisa Habari wa Chama hicho ambapo waliokamatwa ni pamoja na Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na Mbunge wa Viti Maalumu, Zubeda  Sakuru kwa kile kilichoelezwa kuwa ni maagizo aliyopewa ODC wa Nyasa kuwakamata na kuwaweka selo kwa saa 48.

Wengine waliokuwa wamekamatwa ni Philbert Ngatunga (Katibu wa Kanda), Ireneus Ngwatura (M/kiti Mkoa), Delphin Gazia (Katibu Mkoa), Asia Mohamed (Afisa Kanda), Cuthbert Ngwata (M/kiti Wilaya), Charles Makunguru (Mwenezi Wilaya).

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chama hicho amesema “Tumepata taarifa viongozi wentu akiwemo Katibu Mkuu wetu na kuwa kesho wanatakiwa kutipoti, sasa haieleweki ni kwa RPC au ni kwa Mkuu wa Mkoa au kwa mkubwa gani mwengine lakini tumeambiwa kuwa anatakiwa kutipoti mahali.

“Hivi tunavyozungumza utaratibu unafanywa kwa taarifa ambazo sina sababu ya kuzitilia shaka Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu kufikishwa Mahakamani na kushitakiwa kwa kosa kwa kosa la uchochezi”.

Lissu amesema, kuna wanachama wa Chadema zaidi ya 51 Wilayani Chato ambao walidiliki kuifanya mkutano wa ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!