Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtoto afariki baada kula mboga ya majani
Habari Mchanganyiko

Mtoto afariki baada kula mboga ya majani

Spread the love

MTOTO Miriam Michael (6) mkazi wa Ilembo kata Nsalala  wilaya ya Mbeya amefariki dunia baada ya kula mboga za majani zinazodhaniwa kuwa na sumu, anaandika Esther Macha.

Kamanda wa Polisi wa Mkoani Mbeya, Dhahiri Kidavashari amesema kuwa tukio limetokea Juni 13, mwaka huu majira ya saa 18.00 jioni huko Ilembo.

Kidavashari amesema kwamba mtoto huyo alikuwa anasoma chekechea alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa katika hospitali Teule ya Ifisi kwa matibabu.

Akizungumzia zaidi tukio hilo Kidavashari amesema marehemu alifikishwa hospitalini hapo akiwa na mtoto mwenzake aitwaye Felister Mussa (7) wote walifikishwa hospitali kwa ajili ya matibabu.

“Katika tukio hili walikuwa watoto wawili lakini mtoto aliyefariki ni mmoja na huyu mwingine bado yupo hospitali ya Ifisi  anaendelea na matibabu,” amesema Kamanda Kidavashari.

Kamanda wa Polisi wa Mkoani Mbeya, Dhahiri Kidavashari

Aidha Kidavashari amesema kuwa inadaiwa kuwa chanzo cha kifo hicho ni baada ya marehemu na mwenzake kula mboga za majani aina ya maboga ambazo inadaiwa zilipikwa kwenye chombo ambacho kinasadikiwa kilitunzia sumu ya kuulia wadudu ambayo bado haijajulikana.

Hata hivyo kamanda huyo amesema kuwa hali ya kupoteza fahamu ilitokea wakati marehemu na mtoto mwenzake wakicheza baada ya kula na kuanza kulegea na mwili kukosa nguvu.

“Mtoto Felister Mussa bado amelazwa hospitali Teule Ifisi akiendelea na matibabu na hali yake inaendelea vizuri mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi wa kitabibu na kukabidhiwa ndugu kwa mazishi,” amesema Kamanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yashiriki maadhimisho Mei Mosi Arusha

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeungana na maelfu ya...

error: Content is protected !!