Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sheria ya ndoa kurekebishwa kumaliza ndoa za utotoni
Habari Mchanganyiko

Sheria ya ndoa kurekebishwa kumaliza ndoa za utotoni

Dk.Hamisi Kigwangalla, waziri wa Maliasili na Utalii
Spread the love

SERIKALI imesema ipo haja ya kuondoa vifungu vinavyoruhusu ndoa za utotoni kwenye sheria ya ndoa kwa lengo la kumlinda mtoto wa kike na ndoa za utotoni, anaandika Dany Tibason.

Dk. Khamis Kigwangalla, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, alioa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Faida Bakari Mohamed (CCM).

Faida alitaka kujua ni sheria zipi zinazowanyima haki wanawake na watoto nchini na lini serikali itapeleka miswada Bungeni ili kuboresha au kubadilisha Sheria hizo ili ziendane na wakati na kuwapatia haki zao Wanawake na watoto.

Dk. Kigwangallah amesema katia jitihada za kutokomeza ndoa za utotoni mwaka 2016 serikali ilifanyia marekebisho sheia ya elimu ya mwaka 1978 ili kuzia watoto wa shule wasiolewe.

“Kwa mujibu wa Sheria hii Na. 4 ya mwaka 2016 kifungu cha 60A, hairuhusiwi mtu yeyote kuoa ama kumpa ujauzito mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari,” amesema Dk. Kigwangallah

Adha amesema sheria ambazo zimekuwa zikiwanyima haki za urithi ni pamoja nashetia za mirathi za kimila za mwaka 1963 zimekuwa zikiwanyima haki za urithi na umiliki wa ardhi wanawake na watoto.

“Vile vile Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 katika kifungu cha 13 na 17, vinaruhusu mtoto wa kike kuolewa katika umri mdogo wa miaka 14 au 15 kwa ridhaa ya wazazi au mahakama, vifungu hivi pia humnyima mtoto haki za msingi,” alisisitiza.

Katika swali la nyongeza Faida aliihoji serikali kwamba kwa nini isiitambue Mahakama ya Kadhi kama chombo cha waislamu katika masuala ya ndoa ili kuokoa Sheria za kiislam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!