Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliopora ardhi Morogoro kuburuzwa kortini
Habari Mchanganyiko

Waliopora ardhi Morogoro kuburuzwa kortini

Nyundo ya hakimu
Spread the love

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kilosa inatarajia kuwafikisha mahakamani watu 21 wanaodaiwa kujichukulia sheria mikononi na kujimilikisha hekari 66 za kijiji na kujenga nyumba za makazi kwenye eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko, anaandika Christina Haule.

Kesi Mkambala mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo amekiambia kikao maalum cha baraza la madiwani kwamba tayari ameshaamuru nyumba zilizo katika eneo hilo kubomolewa huku watu waliohusika na uvamizi huowakiendelea kushikiliwa na polisi.

“Kundi dogo la watu 21 lilivamia na kujimilikisha eneo la hekari 98 lililoachwa na kijiji kilichopo kata ya Ruhembe. Kijiji kiliomba maeneo hayo na kufanikiwa kupata hekari 32 kati 98 na kufanya hekari 66 kubakia mikononi mwa kundi la watu 21,” amesema.

Mkambala amesema, watu hao wanatarajia kufikishwa mahakamani ili waachie hekari 66 zinazohusisha sehemu ya soko la kijiji na hivyo kuzuia maendeleo ya kijiji hicho.

Aidha Mkambala ameahidi kutembea kila eneo na kwamba endapo atabaini mtu kuvamia eneo lisilo lake atalivunja. “Migogoro haiishi bila kujitoa, nitaendelea kujitoa ili kumliza migogoro ya ardhi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!