Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliopora ardhi Morogoro kuburuzwa kortini
Habari Mchanganyiko

Waliopora ardhi Morogoro kuburuzwa kortini

Nyundo ya hakimu
Spread the love

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kilosa inatarajia kuwafikisha mahakamani watu 21 wanaodaiwa kujichukulia sheria mikononi na kujimilikisha hekari 66 za kijiji na kujenga nyumba za makazi kwenye eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko, anaandika Christina Haule.

Kesi Mkambala mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo amekiambia kikao maalum cha baraza la madiwani kwamba tayari ameshaamuru nyumba zilizo katika eneo hilo kubomolewa huku watu waliohusika na uvamizi huowakiendelea kushikiliwa na polisi.

“Kundi dogo la watu 21 lilivamia na kujimilikisha eneo la hekari 98 lililoachwa na kijiji kilichopo kata ya Ruhembe. Kijiji kiliomba maeneo hayo na kufanikiwa kupata hekari 32 kati 98 na kufanya hekari 66 kubakia mikononi mwa kundi la watu 21,” amesema.

Mkambala amesema, watu hao wanatarajia kufikishwa mahakamani ili waachie hekari 66 zinazohusisha sehemu ya soko la kijiji na hivyo kuzuia maendeleo ya kijiji hicho.

Aidha Mkambala ameahidi kutembea kila eneo na kwamba endapo atabaini mtu kuvamia eneo lisilo lake atalivunja. “Migogoro haiishi bila kujitoa, nitaendelea kujitoa ili kumliza migogoro ya ardhi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!