Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watelekeza mashamba kuwakwepa tembo
Habari Mchanganyiko

Watelekeza mashamba kuwakwepa tembo

Tembo
Spread the love

WANAKIJIJI wa kijiji cha Mtipule kilichopo kata ya Msongozi wilayani Mvomero mkoani hapa wameyatelekeza mashamba yao kwa takribani miaka minne mfululizo wakihofia kuvamia na kuuawa na tembo waharibifu, anaandika Christina Haule.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Luanda Kalunga amesema wanakijiji hao walitelekeza mashamba yao tangu mwaka  2012- 2015 kufuatia Tembo kula na kuharibu mazao yao kila msimu wa kilimo.

Kalunga alikuwa akizungumza katika semina ya kuimarisha ushiriki wa jamii kwa kutunza makazi ya Tembo katika hifadhi ya Taifa ya Mikumi kwenye mradi uliofadhiliwa na mfuko wa misaada wa Uingereza ujulikanao kama The Rufford Foundation (RSG) na unaofanyika kijijini hapo.

“Wakulima wa  kaya  48 za kijiji chetu, walitelekeza mashamba yao kwa miaka minne kwsababu Tembo walikuwa wakivamia na kuwajeruhi wananchi huku wakiharibu mazao wanayoyakuta mashambani ambapo mpaka sasa tayari wameshawauwa watu wawili na kumjeruhi mmoja.

“Waliouawa na Tembo ni pamoja na Josephat John na Emmanuel Valentino ambao wote ni wakulima lakini pia yupo mkulim ninayemkumbuka kwa jin moja la Kazulege, hadi sasa anatumia mipira kupata haja ndogo,” amesema.

Mwenyekiti huyo amesema ana matumini kuwa wakulima watarejea katika mashamba yao watakapopata elimu ya kukabiliana na Tembo kwa kuweka mizinga ya nyuki itakayomfanya Tembo kutopita shambani na kula au kufanya uharibifu wowote.

Ameeleza masikitiko yake juu ya wananchi wanaoharibiwa mazao yao kutolipwa fidia akisema; “Kijiji chetu kipo jirani na hifadhi ya Taifa ya Mikumi, Tembo wanaoharibu mazao yetu na tunajazwa kwenye malipo ya fidia lakini kila mwaka hatulipwi.”

Angelus Runji meneja wa mradi huo, alisema kuwa kufuatia kupata mradi huo wa miezi minane kwenye vijiji vitano vya wilaya za Mvomero na Kilosa watawaelimisha wananchi ili kuondoa dhana mbaya ya wakulima kumchukia Tembo badala yake wamtunze na kumlinda.

“Jamii ya vijiji hivi inaona uwepo wa Tembo ni sawa na janga au shida kubwa tofauti na malengo na matakwa ya Serikali juu ya uhifadhi na ulinzi wa Tembo kama Rasilimali ya Taifa, ni lazima sasa ielimishwe juu y umuhimu wa maliasili zetu ikiwemo wanyama,” amesema Runji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!