Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani yakoleza vita umiliki wa silaha
Kimataifa

Marekani yakoleza vita umiliki wa silaha

Spread the love

BUNGE la Wawakilishi nchini Marekani limeafiki kupigwa marufuku kwa Wamarekani wenye matatizo ya akili kumiliki silaha ikiwa ni jitahada za kukabiliana na uhalifu wa kutumia silaha nchini Marekani, anaandika Wolfram Mwalongo.

Utawala wa Rais Mstaafu Obama ulidhamiria kukomesha umiliki holela wa silaha nchini Marekani, hata hivyo baadhi ya Wabunge kutoka Bunge la Congress walikosoa vikali sheria hiyo kwa kile walichodai sheria hiyo ilitungwa kwaajili ya Wamrekani wote pasipo kuangalia tofauti zao. 

Bob Goodlatte, mwenyekiti wa kamati ya haki amekuwa akikosoa sheria hiyo kwa madai kwamba ni ya kibaguzi kwani hakuna ushahidi wowote unaothibitisha watu wa aina hiyo ndio wanaofanya mashambulizi ya silaha katika taifa hilo.

Itakumbukwa kuwa Donald Trump Rais aliye madarakani kwa sasa, wakati wa kampeni alisema wazi kwamba haoni tatizo la wamrekani kumiliki silaha kwani mashambulizi yanatekelezwa na magaidi. Hata hivyo Bunge la nchi hiyo limeamua tofauti na mtazamo wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!