Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Washukiwa wa dawa za kulevya waanza kujisalimisha
Habari MchanganyikoTangulizi

Washukiwa wa dawa za kulevya waanza kujisalimisha

Babuu wa Kitaa akiwasili kituo cha Polisi cha Kati
Spread the love

TAMKO la Paul Makonda Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam kuwataka watu mbalimbali wanaotuhumiwa kujihusisha biashara au matumizi ya dawa za kulevya kujisalimisha katika Kituo cha Polisi cha Kati limeitikiwa na baadhi ya watu hao, anaandika Faki Sosi.

Makonda alitaja majina ya watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya ambao tayari wamekamatwa, wanaotakiwa kukamatwa na kuwekwa rumande kupisha uchunguzi pamoja na wanaotakiwa kufika polisi kwa ajili ya kuhojiwa.

Mapema leo asubuhi, saa 4:35 Babuu wa Kitaa ambaye ni mtangazaji maarufu wa kituo cha Clouds TV alikuwa mtu wa kwanza kufika Kituo cha Polisi cha Kati akiitikia wito uliotolewa na Mkuu wa Mkoa. Babuu aliingia katika eneo hilo akionekana mwenye kujiamini huku akitabasamu wakati waandishi wa habari wakimpiga picha.

Baadaye Khalid Mohamed maarufu kama TID, ambaye ni msanii maarufu wa muziki wa RnB aliwasili kituoni hapo. TID alifika saa 5:07 asubuhi, akiwa amevaa miwani, shati nyeusi na suruali nyeupe.

Hamidu Chambuso maarufu kama ‘Nyandu tozi’ au Dogo Hamidu, msanii wa Hiphop aliingia katika eneo la polisi saa 5:37 asubuhi. Nyandu alizua gumzo baada ya kuingia huku akiwa amevaa kanzu nyeupe na kofia na kuwapita waandishi na wapiga picha bila kumtambua.

Waandishi walishituka na kumtambua baada ya kuingia ndani ya eneo la kituo cha polisi na kuulizia pa kuelekea.

Hamidu Chambuso aka Nyandu Toz akiwasili kituo cha Polisi cha Kati

Baadaye Wema Sepetu, msanii wa filamu na miss Tanzania mwaka 2006 aliwasili katika kituo hicho akiwa amejisitiri kwa vazi refu na kujifunika kwa mtandio mweusi kichwani.

Wema Sepetu akiwasili kituo cha Polisi cha Kati

Baadhi ya wasanii maarufu ambao mpaka sasa bado hawajafika kituoni na waliagizwa kufanya hivyo na Makonda ni pamoja na Rashid Makwiro (Chid Benz), Heri Samir (Mr. Blue) na Rachel maarufu kama Rachel Kizunguzungu.

MwanaHALISI Online itaendelea kukuletea taarifa za moja kwa moja kutoka Kituo cha Polisi cha Kati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

error: Content is protected !!