Monday , 5 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani yakoleza vita umiliki wa silaha
Kimataifa

Marekani yakoleza vita umiliki wa silaha

Spread the love

BUNGE la Wawakilishi nchini Marekani limeafiki kupigwa marufuku kwa Wamarekani wenye matatizo ya akili kumiliki silaha ikiwa ni jitahada za kukabiliana na uhalifu wa kutumia silaha nchini Marekani, anaandika Wolfram Mwalongo.

Utawala wa Rais Mstaafu Obama ulidhamiria kukomesha umiliki holela wa silaha nchini Marekani, hata hivyo baadhi ya Wabunge kutoka Bunge la Congress walikosoa vikali sheria hiyo kwa kile walichodai sheria hiyo ilitungwa kwaajili ya Wamrekani wote pasipo kuangalia tofauti zao. 

Bob Goodlatte, mwenyekiti wa kamati ya haki amekuwa akikosoa sheria hiyo kwa madai kwamba ni ya kibaguzi kwani hakuna ushahidi wowote unaothibitisha watu wa aina hiyo ndio wanaofanya mashambulizi ya silaha katika taifa hilo.

Itakumbukwa kuwa Donald Trump Rais aliye madarakani kwa sasa, wakati wa kampeni alisema wazi kwamba haoni tatizo la wamrekani kumiliki silaha kwani mashambulizi yanatekelezwa na magaidi. Hata hivyo Bunge la nchi hiyo limeamua tofauti na mtazamo wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love  SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza...

error: Content is protected !!