Tuesday , 7 May 2024
Habari za Siasa

Chadema, CCM vyaonywa

Dk. Steven Kebwe, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro
Spread the love

VYAMA vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro vimeonywa, anaandika Christina Haule.

Vyama hivyo vimetakiwa kujiepusha na vitendo vya vurugu wakati huu wa kampeni za udiwani zinazotarajiwa kukoma tarehe 21 Januari mwaka huu ambapo tarehe 22 Januari uchaguzi utafanyika.

Wito huo umetolewa na Dk. Steven Kebwe, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana.

Amesema kuwa, mkoa huo hautavumilia kuona chama chochote kinakiuka masharti ya uchaguzi huo kwa namna yoyote ile.

Dk. Kebwe amewashauri wananchi kuwa watulivu katika kipindi cha kampeni na kuwataka kusikiliza maelezo yanayotolewa na vyama vyote ili waweze kuchagua kiongozi watakayemuona anafaa kuwaletea maendeleo ya kweli.

Wakati huohuo Dk. Kebwe amesema kuwa, zoezi la upigaji chapa mifugo linatarajiwa kuanza kufanyika tarehe 1 Februari mwaka huu baada ya mwanzo kusitishwa kutokana na jamii ya wafugaji kutoa ushirikiano wa kutosha na baadhi ya mifugo kudaiwa kuumia kutokana na chapa hizo.

“Zoezi hili ni utekelezaji wa agizo la waziri mkuu kwa barua kumbukumbu namba PM/P/2/569/42, hivyo tunaomba ushirikiano toka kwa makundi yote, ndugu zetu wafugaji na wananchi wote wa mkoa wa Morogoro,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!