Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Uganda kuivaa Ghana leo AFCON
Michezo

Uganda kuivaa Ghana leo AFCON

Kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda 'The Crances'
Spread the love

TIMU ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’ leo itatupa karata yake ya kwanza kwenye michuano ya kombe la mataifa Afrika (AFCON) inayofanyika nchini Gabon dhidi ya timu ya taifa ya Ghana ‘The Black Stars’ kwenye mchezo wa kundi D.

Uganda ndio timu pekee iliyofanikiwa kufuzu michuano hiyo kutokea ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, ambao ulikuwa hauna mwakilishi katika michuano hiyo katika kipindi cha muda mrefu kutokana na timu zake kutofanya vizuri katika michezo ya kufuzu.

Mchezo huo ambao unatazamiwa kuwa mgumu kwa pande zote mbili kutokana na ubora wa wachezaji na vikosi walivyokuwa navyo, Ghana inafahamika ni timu ngumu na yenye uzoefu katikia michuano hiyo kwa miaka ya hivi karibuni kutokana kuwa na wimbi kubwa la wachezaji wanaocheza katika ligi kubwa barani Ulaya.

Mechi nyingine itakayopigwa katika kundi hilo leo, itazikutanisha timu za Mali dhidi ya Misri majira ya saa nne usiku, na itatoa msimamo kamili wa kundi hilo ambalo linaonekana kuwa gumu kutokana na ubora wa timu zilizopo humo.

Uganda ambayo kwa sasa inafuzu michuano hiyo kwa mara ya pili, toka mwaka 1978, imekuwa na mafanikio makubwa kwenye soka kwa siku za hivi karibuni kiasi cha kushinda tuzo ya timu bora ya CAF katika hafla iliyofanyika Nigeria, huku mlinda mlango wao namba moja Denis Onyango akitwaa tuzo ya mchezaji bora kwa wanaocheza ligi ya ndani Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

error: Content is protected !!