Monday , 5 June 2023
Habari za Siasa

Chadema, CCM vyaonywa

Dk. Steven Kebwe, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro
Spread the love

VYAMA vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro vimeonywa, anaandika Christina Haule.

Vyama hivyo vimetakiwa kujiepusha na vitendo vya vurugu wakati huu wa kampeni za udiwani zinazotarajiwa kukoma tarehe 21 Januari mwaka huu ambapo tarehe 22 Januari uchaguzi utafanyika.

Wito huo umetolewa na Dk. Steven Kebwe, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana.

Amesema kuwa, mkoa huo hautavumilia kuona chama chochote kinakiuka masharti ya uchaguzi huo kwa namna yoyote ile.

Dk. Kebwe amewashauri wananchi kuwa watulivu katika kipindi cha kampeni na kuwataka kusikiliza maelezo yanayotolewa na vyama vyote ili waweze kuchagua kiongozi watakayemuona anafaa kuwaletea maendeleo ya kweli.

Wakati huohuo Dk. Kebwe amesema kuwa, zoezi la upigaji chapa mifugo linatarajiwa kuanza kufanyika tarehe 1 Februari mwaka huu baada ya mwanzo kusitishwa kutokana na jamii ya wafugaji kutoa ushirikiano wa kutosha na baadhi ya mifugo kudaiwa kuumia kutokana na chapa hizo.

“Zoezi hili ni utekelezaji wa agizo la waziri mkuu kwa barua kumbukumbu namba PM/P/2/569/42, hivyo tunaomba ushirikiano toka kwa makundi yote, ndugu zetu wafugaji na wananchi wote wa mkoa wa Morogoro,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!