Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa 41 wafa kwa ajali ya moto jela
Kimataifa

41 wafa kwa ajali ya moto jela

Spread the love

 

MOTO uliozuka usiku wa manane katika gereza lenye msongamano mkubwa wa wafungwa huko Jakarta, nchini Indonesia umesababisha vifo vya watu 41 na wengine kadhaa wamejeruhiwa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi nchini humo imesema moto huo ulizuka mapema leo asubuhi tarehe 8 Septemba, katika gereza la Tangerang lililopo magharibi mwa mji mkuu wa Indonesia.

Mkuu wa Polisi wa Jakarta, Fadil Imran amewaambia waandishi wa habari moto huo umetokea upande wa Block C ambapo ndipo moto ulipozuka kulikuwa na jumla ya wafungwa 122 ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi zinazohusiana na madawa ya kulevya.

“Wafungwa 41 wamefariki dunia, wanane wamejeruhiwa vibaya na 72 wana majeraha madogo,”

Picha za televisheni zimeonyesha maofisa wa idara ya Zima moto wamekabiliana na moto ulioteketeza moja ya majengo ya gereza, ukitoa wingu zito la moshi.

Maofisa wa zima moto wamedhibiti moto huo ambao uliathiri moja ya majengo ya jela hilo, wanakozuiliwa hasa wafungwa waliohukumiwa kwa biashara au utumiaji wa dawa za kulevya.

Mamlaka bado wanachunguza sababu za moto, lakini wengi wamebaini kwamba moto huo ulisababishwa na hitilafu zinazotokana na mifumo duni ya umeme.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!