Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vifungashio vya mawese tayari, Serikali yatoa maagizo
Habari za Siasa

Vifungashio vya mawese tayari, Serikali yatoa maagizo

Mafuta ya mawese
Spread the love

 

SHIRIKA la Kuhudumia Viwanda Vidogo (Sido), Mkoa wa Kigoma limetengeneza sampuli ya vifungashio vya mafuta ya Mawese vitakavyotumiwa na wakulima wa mafuta hayo. Anaripoti Helena Mkonyi, TUDARCo … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumatano, tarehe 8 Septemba 2021 na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigai wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Assa Nelson.

Nelson alitaka kujua serikali imefikia hatua gani kurekebisha vifungashio vya mafuta ya Mawese kwa kuwa wananchi wanaumizwa na kunyonywa kupitia vifungashio vinavyotumika sasa.

Kingai akijibu swali hilo amesema, Sido imetengeneza sampuli ya vifungashio vitakavyotumika kufungashia mafuta ya Mawese ambapo imetengeneza vifungashio vya mafuta lita tano, lita 20 na vifungashio hvivo vipo katika mfumo wa ndoo za chuma.

Pia, naibu waziri huyo amesema, vifungashio hivo vipo tayari na kwamba hatua inayofuata ni kuwasilisha sampuli ya vifungashio hivyo kwa Wakala wa Vipimo (WMA) kwa ajili ya uhakiki na mara baada ya uhakiki huo vifungashio hivyo vitawasilishwa Sido ili viweze kuzalishwa kwa wingi kwa ajii ya kufungashia mafuta hayo.

Zao la chikichi inayotoa mafuta ya mawese

Ametumia fursa hiyo, kutoamaagizo kwa Sido ikishiriakana na WMA kuharakisha uzalishaji wa vifungashio.

Amesema, vizalishwe kwa wingi na endapo kutakuwa na baadhi ya marekebisho kutoka kwa wakala wa vipimo, marekebisho ya vifungashio hivyo yatolewe kwa haraka ili wakulima wa Mawese wasiendelee kunyonywa kama ilivyokuwa mwanzo.

Kutokana na majibu hayo, baadhi ya wabunge wameuliza maswali ikiwemo ni mikakati gani serikali imeweka katika kutekeleza mambo yaliyoombwa na wananchi kufanyiwa kazi na waziri mkuu?

Pia, swali jingine ni je, ni lini vifungashio rasmi vya viazi vitapatikana kwa wakulima wa viazi Makete?

Majibu ya swali la kwanza, Kingai amesema, serikali imezisikia changamoto zote zinazowakabili wakulima wote na inaanza mikakati mbalimbali ya kutatua changamoto izo kwa wakulima.

Swali la pili ni kwamba serikali imeunda timu maalumu na timu hiyo inapaswa ije na mikakati maalumu ya vifungashio vya mazao maalamu na sio viazi tu ili kuepusha unyonyaji uliopo kwa wakulima.

1 Comment

  • Asante sana kwa hilo.

    Ninaamini vitatufikia na huku Mbeya (Rungwe Na Kyela), na Tabora (Urambo). Hizi sehemu nazo wanalima zao la Michikichi.

    Rafiki yako,

    Aliko Musa.

    Real Estate Investment Consultant

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!