Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko 21 wadakwa kwa tuhuma wizi vifaa vya miundombinu ya maji
Habari Mchanganyiko

21 wadakwa kwa tuhuma wizi vifaa vya miundombinu ya maji

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora, Richard Abwao
Spread the love

 

JESHI la Polisi Mkoani Tabora limewanasa watu 21 kwa tuhuma ya kujihusisha na wizi wa vifaa vya na miundombinu ya maji mali ya Mamlaka ya maji Safi na Usafi wa Mazingira mkoani Tabora (TUWASA). Anaripoti Paul Kayanda, Tabora … (endelea).

Akizungumza jana tarehe 19 Aprili 2023 na waandishi wa habari mkoani Tabora. Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Richard Abwao amesema hatua hiyo imefanikishwa na kikosi kazi cha wilaya ya Tabora kilichoundwa kwa kushirikisha askari polisi na watumishi TUWASA.

Pia amesema katika operesheni hiyo, askari walikamata vitu vilivyoibiwa ambavyo ni pamoja na nondo 353, connector mbili, koki 43, gate valve 11, stand za mita ya maji mbili, vipande vya bomba3/4 21, valve handle moja, vipande vya bomba za barabarani 12, binding wire moja, bomba 33, mizani ndogo moja, bati tatu na vitanda viwili vya chuma vya friji za mochwari.

Ameongeza kuwa baada ya upelelezi kukamilika watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazowakabili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!