Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Uswatini afariki dunia
Kimataifa

Waziri Mkuu Uswatini afariki dunia

Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Uswatini, Ambrose Dlamini, amefariki dunia jana Jumapili tarehe 13 Desemba 2020, hospitalini nchini Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Jumapili na Naibu Waziri Mkuu wa Uswatini, Themba Masuku ilieleza, Dlamini mwenye miaka 52, alifikwa na mauti wakati akiendelea na matibabu.

Katika taarifa hiyo, Masuku hakueleza chanzo cha kifo cha Dlamini, aliyekuwa waziri mkuu kuanzia 27 Oktoba 2018.

Hata hivyo, hivi karibuni, waziri mkuu huyo, alipimwa na kukutwa na maambukizo ya virusi vya corona (COVID-19).

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametuma salamu za rambirambi kwa familia, marafiki na wananchi wa Uswatini kutokana na kumpoteza kiongozi wao na kuwataka kuwa watulivu katika kipindi hiki cha maombolezo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!