DROO ya michuano ya Klabu Bingwa Ulaya (Uefa) imechezeshwa hii leo ambapo klabu ya Liverpool itawavaa vigogo wa Ujerumani RB Leipzing ambao waliwaondosha Manchester United kwenye hatua ya makundi mara baada ya kupata ushindi wa mabao 3-2. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
RB Leipzing ambao walishika nafasi ya pili kwenye kundi H, wakiwa na pointi 12 watacheza mchezo wa kwanza dhidi ya Liverpool wakiwa nyumbani kwenye dimba la Red Bull Arena nchini Ujerumani.
Liverpool ambao wamevuka hatua hiyo mara baada ya kuwa vinara kwenye kundi D, mbele ya Atalanta, Ajax na Midtyjland.
Michezo mingine kwenye kundi hiyo itawakutanisha Barcelona dhidi ya PSG, Lazio kuwakabili Bayern Munchen, Porto dhidi ya Juventus, Sevilla kuwakabili Dortumund, Atalanda itawakaribisha Real Madrid, huku Atletico Madrid watawavaa Chelsea kwenye mchezo wa kwanza.
Fainali za michuano hiyo zinatarajiwa kuchezwa mwakani kwenye jiji la Instabul, Uturuki huku mabingwa watetezi wakiwa ni Bayern Munchen.
Leave a comment