Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Uswatini afariki dunia
Kimataifa

Waziri Mkuu Uswatini afariki dunia

Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Uswatini, Ambrose Dlamini, amefariki dunia jana Jumapili tarehe 13 Desemba 2020, hospitalini nchini Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Jumapili na Naibu Waziri Mkuu wa Uswatini, Themba Masuku ilieleza, Dlamini mwenye miaka 52, alifikwa na mauti wakati akiendelea na matibabu.

Katika taarifa hiyo, Masuku hakueleza chanzo cha kifo cha Dlamini, aliyekuwa waziri mkuu kuanzia 27 Oktoba 2018.

Hata hivyo, hivi karibuni, waziri mkuu huyo, alipimwa na kukutwa na maambukizo ya virusi vya corona (COVID-19).

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametuma salamu za rambirambi kwa familia, marafiki na wananchi wa Uswatini kutokana na kumpoteza kiongozi wao na kuwataka kuwa watulivu katika kipindi hiki cha maombolezo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!