Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Uswatini afariki dunia
Kimataifa

Waziri Mkuu Uswatini afariki dunia

Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Uswatini, Ambrose Dlamini, amefariki dunia jana Jumapili tarehe 13 Desemba 2020, hospitalini nchini Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Jumapili na Naibu Waziri Mkuu wa Uswatini, Themba Masuku ilieleza, Dlamini mwenye miaka 52, alifikwa na mauti wakati akiendelea na matibabu.

Katika taarifa hiyo, Masuku hakueleza chanzo cha kifo cha Dlamini, aliyekuwa waziri mkuu kuanzia 27 Oktoba 2018.

Hata hivyo, hivi karibuni, waziri mkuu huyo, alipimwa na kukutwa na maambukizo ya virusi vya corona (COVID-19).

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametuma salamu za rambirambi kwa familia, marafiki na wananchi wa Uswatini kutokana na kumpoteza kiongozi wao na kuwataka kuwa watulivu katika kipindi hiki cha maombolezo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!