Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanaharakati wazidi kumsakama mke wa Mugabe
Kimataifa

Wanaharakati wazidi kumsakama mke wa Mugabe

Mwanamitindo Gabriella Engels aliyeshambuliwa na Grace Mugabe
Spread the love

GABRIELLA Engels, mwanamitindo nchini Afrika Kusini aliyeshambuliwa na Grace Mugabe, mke wa Rais wa Zimbabwe, amepinga kinga ya kidiplomasia inayotolewa na serikali ya nchi yake kwa vigogo, anaandika Irene Emmanuel.

Binti huyo mwenye umri wa miaka 20 anaungwa mkono na kundi la shinikizo, AfriForum, ambalo katika kupinga sheria hiyo wameonyesha ukurasa wa kwanza wa fomu ya maombi kutoka mahakama kuu ya mji mkuu na kudai kwamba waziri wa mambo ya nje, Maite Nkoana Mashabane ameelezea sheria ya kinga ya kidiplomasia vibaya.

AfriForum wamedai kuwa sheria hiyo ya kidiplomasi inayowakinga vigogo na serikali haihusishi vigogo ambao wamesababisha vifo au majeraha kwa wananchi wake.

Polisi wa Afrika Kusini wamesema Grace hajaripoti kituoni kama ambavyo ilikuwa imepangwa na ameondoka nchini na mume wake Robert Mugabe jumapili iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!