Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliouawa kanisani Sri Lanka wafika 290
Kimataifa

Waliouawa kanisani Sri Lanka wafika 290

Spread the love

MIILI ya watu waliopoteza maisha katika shambulio la kigaidi kwenye makanisa matatu na hoteli za kifahari nchini Sri Lanka, imefikia 290. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Shambulizi la mabomu katika makanisa yaliyoko Negombo, Batticaloa na Wilaya ya Colombo Kochchikade pamoja na hoteli za Shangri-La, Kingsburry na Common Grand yalitokea wakati wa ibada ya Sikuu ya Pasaka majira ya asubuhi jana tarehe 21 Aprili 2019.

Vyombo vya Habari vya Kimataifa vimeripoti kwamba, takribani watu 500 wamejeruhiwa kwenye shambulio hilo, na kwamba Jeshi la Polisi linawashikilia watu 24 wanaoshukiwa kuhusika na tukio hilo.

Taarifa za vyombo hivyo zinaeleza kwamba, mamlaka nchini Srilanka viliarifiwa wiki mbili kabla taarifa za tishio la kiusalama.

Katibu wa Masuala ya Ulinzi SriLanka, Hemasari Fernando amewataka wananchi wa taifa hilo kutovilaumu vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutozuia shambulizi hilo, akisema kwamba licha ya uwepo wa taarifa za matishio ya kiusalama, vyombo hivyo havikudhania kama magaidi wangetekeleza katika maeneo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!