Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Telegram kudhibiti Magaidi Indonesia
Kimataifa

Telegram kudhibiti Magaidi Indonesia

Mtandao wa Telegram
Spread the love

MTANDAO wa kijamii wa Telegram, umeahidi kuwa utafunga akaunti zinazohusiana na ugaidi nchini Indonesia, anaandika Hamisi Mguta.

Maamuzi hayo ni kufuatia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia nchini humo kufunga huduma za mtandao huo nchini humo siku ya Ijumaa kwa kudai kuwa Telegram imetumiwa kuunga mkono itikadi kali na kutoa maelekezo ya kufanya mashambulizi.

Taarifa kupitia BBC zinaeleza kuwa Pavel Durov, Mwanzilishi wa mtandao huo kupitia taarifa yake amesema kuwa Telegram sasa imeondoa akaunti zote zinazohusika na ugaidi zilizotajwa na serikali.

Pavel Durov, Mwanzilishi wa Mtandao wa Telegram

Hatua hiyo inakuja huku kukiwa na wasiwasi wa kuibuka kwa kundi la Islamic State kusini mashariki mwa Asia ambalo limedai kuhusika kwenye mashambulizi kadhaa nchini Indonesia mwaka huu na limepigana na jeshi mjini Marawi katika kisiwa cha mindanao nchini Ufilipino.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!