Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtoto wa miaka mitano afariki kwa moto
Habari Mchanganyiko

Mtoto wa miaka mitano afariki kwa moto

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, ACP Jonathan Shanna
Spread the love

MTOTO wa miaka mitano, Solile Emannuel amefariki dunia katika ajali ya moto iliyotokea tarehe 3 Oktoba 2018 nyumbani kwao maeneo ya Nh’obola wilayani Nayamaga mkoa wa Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kuhusu tukio hilo leo tarehe 6 Oktoba 2018, Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, ACP Jonathan Shanna amesema chanzo cha moto huo ni kuungua kwa godoro kulikosababishwa na marehemu alipokuwa anachezea njiti ya kiberiti.

Kamanda Shanna ameeleza kuwa, wakati mtoto huyo anafanya tukio hilo, aliachwa peke yake na wazazi wake waliokuwa bustanini wakilima.

“Tukio hilo limetokea tarehe 3 saa 17:00 jioni, wakati marehemu alipoachwa peke yake chumbani akila chakula huku wazazi wake wakiwa bustanini wakilima. Inadaiwa marehemu alikuwa akichezea njiti ya kiberiti na kupelekea kuwasha moto ulioanza kuunguza godoro, nguo na hatimaye kushika nyumba nzima hali iliyopelekea marehemu kukosa hewa na baadae kufariki dunia,” ameeleza Kamanda Shanna.

Amesema, baada ya tukio hilo kutokea, Jeshi la Polisi lilifika kwa haraka eneo la tukio na kushirkiana na wananchi kutoa msaada, lakini moto ulikuwa tayari umepoteza uhai wa mtoto na kutekeza mali na vitu vyote katika nyumba hiiyo.

“Thamani ya mali na vitu vilivyoteketea katika ajali hiyo bado haijafahamika. Mwili wa marehemu tayari umefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi,” amesema.

Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, limewasisitiza wazazi na walezi kuwa waangalifu na watoto wakati wote, na waache tabia ya kuwaacha watoto kwenye nyumba peke yao kwani kunaweza kuhatarisha usalama wao na baadae kupata majeruhi au kufariki dunia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!