Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkuu wa Usalama Shirika la Posta atoweka kusikojulikana
Habari Mchanganyiko

Mkuu wa Usalama Shirika la Posta atoweka kusikojulikana

Spread the love

SHIRIKA la Posta Tanzania (TPC) linamsaka Mkuu wake wa Kitengo cha Usalama, George Mwamgabe anayedaiwa kutoweka kusiko julikana wiki moja iliyopita. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

TPC imefikia uamuzi huo baada ya Mwamgabe kutoonekana ofisini kwake kwa muda mrefu bila ya kutoa taarifa yoyote, ambapo ilimtafuta kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo nyumbani kwake pasipo mafanikio.

Taarifa ya TPC iliyotolewa na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa shirika hilo, Joseph Ngowi imemtaka Mkuu huyo wa Usalama kuhudhuria kwenye kikao cha nidhamu kilichoitishwa, ambacho kinatarajiwa kufanyika tarehe 1 Novemba 2018 katika ofisi  za makao makuu ya TPC, kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili.

Taarifa ya Ngowi inaeleza kuwa, kama Mwamgabe hatahudhuria kikao hicho pamoja na kutotoa taarifa kwa mwajiri wake, TPC itaendelea na kikao hicho ikiwemo maamuzi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!