NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dk. Hamis Kigwangala ametoa miezi mitatu kwa halmashauri ya mji wa Kahama kuhakikisha inafanya ukarabati wa chumba cha upasuaji katika hospitali ya mji wa Kahama, anaandika Mwandishi Wetu
Ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo yenye lengo la kutembelea baadhi ya sehemu zinazotoa huduma za afya.
Akiwa hospitalini hapo Dk. Kigwangala amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Kahama, Anderson Msumba kuhakikisha anasimamia kazi hiyo kwa weledi ili liweze kufanikiwa.
Pia amemtaka Mkurugenzi kuhakikisha anafanya marekebisho katika chumba cha kujifungulia akina mama wajawazito.
Leave a comment