Saturday , 2 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani na Korea wazidi kuvimbiana
Kimataifa

Marekani na Korea wazidi kuvimbiana

Mifano ya makombora ya Scud yanayomilikiwa na Korea Kaskazini
Spread the love

Rex Tellerson, Waziri wa Mambo ya Kigeni  Nchini Marekani amejibu juu ya jaribio la pili la kombora la masafa marefu lililofanywa na Korea Kaskazini, anaandika Irene Emmanuel.

“Sisi si maadui zenu, sisi si tisho kwenu , lakini mnatuwekea tisho lisilo kubalikana lazima tujibu.” Amesema Tellerson.

ameyasema hayo baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la pili la kombora la masafa marefu linalojulikana kama Inter-continental Ballistic Missile (ICBM), tar 28 julai linaloweza kushambulia bara jingine.

“Hatutaki mabadiliko ya utawala, hatulengi kuuangusha utawala, hatutaki kuharakisha muungano wa eneo la Peninsula, hatutaki sababu ya kutuma wanajeshi wetu kwenye eneo lenu.” Amesema Tillerson, akimaanisha mpaka baina ya Korea kaskazini na Korea Kusini.

Ikumbukwe kuwa Donald Trump, Rais wa Marekani aliwahi kumwambia  Seneta wa Chama cha Republican kuwa kunaweza kuwa na vita dhidi ya Korea Kaskazini kama mpango wao wa makombora utaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

Kimataifa

Mateka wa Israel, Gaza kuanza kuachiwa leo

Spread the loveMakubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na vikosi vya...

Kimataifa

Israel, Hamas kusitisha mapigano kwa muda

Spread the loveNCHI ya Israel, pamoja na kikundi cha wanamgambo wa kiislamu,...

error: Content is protected !!