Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Anywesha watoto sumu kwa wivu wa mapenzi
Habari Mchanganyiko

Anywesha watoto sumu kwa wivu wa mapenzi

Spread the love

SELEMANI Mashaka Haruna (31), Mkazi wa Majengo wilayani Urambo, Tabora anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuuwa mtoto wake kwa sumu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

Akizungumza kuhusu tukio hilo leo tarehe 30 Aprili 2019, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Emmanuel Nley amesema, tukio hilo la kusikitisha lilitokea jana.

Kamanda Nley amesema, Haruna anadaiwa kuwapa watoto wake wa kufikia soda yenye sumu, ambapo mmoja aliyefahamika kwa jina la Nyamizi Ally (7) amefariki huku Kalunde Ally (4) akidhurika.

Kamanda Nley amesema, uchunguzi wa awali umebaini kwamba, chanzo cha mtuhumiwa huyo kuwanywesha sumu watoto wake wa kufikia ni wivu kwa kuwa, alikua hataki kuishi na watoto hao.

“Tarehe 29 Aprili 2019 majira ya mchana Jeshi la Polisi tulipata taarifa ya tukio hilo, tulifika kwa mtuhumiwa na kumkamata . Uchunguzi wa awali unaonesha alikuwa na chuki na watoto wake wa kufikia, alitaka waende kwa baba yao,” amesema Kamanda Nley.

Kamanda Nley amesema uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea na kwamba ukikamilika hatua zaidi za kisheria zitachukukiwa dhidi ya mhusika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!