Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo SportPesa yaikutanisha Simba na Sevilla
Michezo

SportPesa yaikutanisha Simba na Sevilla

Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetegua kitendawili cha nani atakayecheza na timu ya Sevilla ya Hispania iliyoalikwa kuja kucheza na timu mojawapo nchini inayodhaminiwa na SportPesa. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Akizungumza na waandishi wa Habari leo tarehe 30 Aprili mwaka 2019 Wilfred Kidau, Katibu Mkuu wa (TFF) amesema kuwa SportPesa imefikisha mezani rai ya kuzichezesha Simba na Yanga ili mshindi acheze na Klabu hiyo iliyoalikwa kutoka nchini Hispania.

Kidau amesema kulingana na ufinyu wa ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara wameamua timu ya Simba ndiyo itakayocheza na Sevilla.

Amesema kuwa uamuzi huo ni zao la majadiliano yao na  SportPesa ambapo tayari utararibu wa mchezo huo ushapangwa.

Abass Tarimba, Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa amesema kuwa mchezo huo utakaochezwa tarehe 23 Mei, 2019 kati ya Simba na Sevilla ni fursa kwa Tanzania na klabu hiyo kujionesha kimataifa.

Amesema kuwa mechi hiyo itarushwa kwa matangazo ya moja kwa moja na televisheni kubwa duniani hiyo ni kutokana na ukubwa na timu ya Sevilla.

Amesema kuwa sasa ni wakati kwa Tanzania na Serikali kuitangaza nchi kwenye sekta ya utalii licha ya kuweka wazi kuwa tayari washafanya mazungumzo na Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangalah kuhusu utayarishaji wa mazingira ya kitangaza nchi kwenye sekta ya utalii.

Amesema kuwa matokeo Everton kufika nchini yalionekana baada ya mchezo ule wachezaji nyota wengi kama David Beckham walifika nchini kwa ajili ya kufanya utalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!