Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Katiba ACT-Wazalendo haijavunjwa, ‘tumpigie kura Lissu’
Habari za Siasa

Zitto: Katiba ACT-Wazalendo haijavunjwa, ‘tumpigie kura Lissu’

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Zuberi Kabwe, Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, ameendelea kuwaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi tarehe 28 Oktoba 2020 kumpigia kura Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Jumatano tarehe 21 Oktoba 2020, Zitto amesema, uamuzi wa kumuunga mkono Lissu ni “maamuzi ya chama kwa mujibu wa vikao.”

Zitto ambaye pia ni mgombea ubunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT-Wazalendo amesema katika uamuzi huo wa kumuunga mkono LIssu, katiba ya chama hicho haijavunjwa wala kukiukwa.

Benard Membe, Mgombea Urais kwa tiketi ya ACT-Wazalendo

Katika kusisitiza adhima ya kumuunga mkono Lissu, Zitto amesema, “Watanzania waende kupiga kura kwa wingi na wampigie Tundu Lissu kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.”

Zitto na Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo wametangaza licha ya kumsimamisha mgombea urais, Bernard Membe lakini kama chama wameona Lissu ana nguvu za kumtoa mgombea wa CCM, Rais John Pombe Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!