KAMATI ya Maadili Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam imemfungia mgombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia ACT-Wazalendo, Saed Kubenea, kufanya kampeni kwa muda wa siku saba, kuanzia leo hadi 27 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Adhabu hiyo dhidi ya Kubenea, imetolewa jana Jumanne tarehe 20 Oktoba 2020, akituhumiwa kwa makosa ya ukiukwaji wa maadili dhidi ya mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abbas Gulam Tarimba.
Kubenea amekutana na adhabu hiyo zikiwa zimebaki takribani siku saba kabla ya siku ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.
Leave a comment