Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto akamatwa, Mdee…
Habari za Siasa

Zitto akamatwa, Mdee…

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam nchini Tanzania, limemkamata Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe akiwa Kituo cha Polisi Osterbay jijini humo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Zitto amekamatwa leo mchana Jumanne tarehe 3 Novemba 2020 akiwa kituoni hapo alipokwenda kuwajulia hali, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na wenzake wanaoshikiliwa kituoni hapo.

Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano kwa Umma wa ACT-Wazalendo, Janeth Rithe amesema, “ni kweli Zitto amekamatwa na polisi akiwa kituo cha polisi cha Oysterbay alikokwenda kuwaona viongozi wa Chadema.”

          Soma zaidi:-

Zitto aliyekuwa mgombea ubunge wa Kigoma Mjini amekamatwa saa chache kupita tangu, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa kutangaza kumtafuta Zitto na Halima Mdee, aliyekuwa mgombea ubunge Kawe, Dar es Salaam kupitia Chadema.

Kamanda Mambosasa aliwataka wawili hao kujisalimisha polisi kwa mahojiano dhidi ya tuhuma zinazowakabili.

Kukamatwa kwa Zitto kumebakisha Mdee, ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!