Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto aipa ushauri Serikali maandalizi dira mpya ya maendeleo
Habari za Siasa

Zitto aipa ushauri Serikali maandalizi dira mpya ya maendeleo

Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameishauri Serikali ianzishe mjadala wa kitaifa kwa ajili ya kujadili namna ya kuandaa dira mpya ya maendeleo kwa miaka 25 ijayo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Zitto ametoa ushauri huo katika mkutano wa maafisa mipango na wachumi wa wizara, idara, mashirika ya umma, mikoa na mamlaka za serikali za mitaa nchi nzima, uliofanyika jijini Arusha, kwa ajili ya kujadili maandalizi ya dira ya taifa ya maendeleo.

“Lazima tuwe na mjadala wa ukweli miongoni mwetu Watanzania bila ubaguzi wa kisiasa kuhusu miaka 25 iliyopita. Je tulikuwa na mwafaka wa kitaifa kuhusu dira? Je, tulikuwa na nidhamu ya kutosha kutekeleza dira ya 2025? Kwanini ilichukua miaka 10 kuanza kutekeleza dira? Tuwe tayari kukubali matobo na kuweka mikakati ya kuziba matobo hayo,” amesema Zitto.

Mwanasiasa huyo amesema kuwa, baada ya mjadala huo kufanyika, mwafaka wa kitaifa ujenge juu ya namna ya kuipeleka Tanzania katika miaka 25 ijayo.

“Lazima na ni muhimu kwa Watu wenye kufanya maamuzi na wenye ushawishi wa kimaamuzi  kukubaliana mwafaka wa kitaifa. Hii bargain – ijenge makubaliano ya uhakika kuhusu maendeleo , kujenga dola lenye utayari wa kusaidia maendeleo na sio predatory state, ikubali kujifunza na kurekebisha makosa kila wakati yakitokea,” amesema Zitto.

Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo, amesema kuna haja ya Serikali kuweka mikakati itakayosaidia kukuza uchumi wanchi kwa wastani wa asilimia nane kila mwaka, ili kukidhi ongezeko la idadi ya watu inayokadiriwa kufikia milioni 130 ifikapo 2050

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!