Klabu ya Yanga ipo mbioni hivi karibuni kumtambulisha mchezaji mwengine mpya atakayejiunga na timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao wa mashindano. Anaripoti Wiston Josia/ TUDARCo(endelea…)
Kikosi hicho ambacho kwa sasa kimekita kambi nchini Morocco, kikiwa na siku mbili toka kianze mazoezi jana Agosti 17, 2021.
Akizungumza na Azam TV, akiwa nchini Morocco, makamu Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ndani ya klabu ya Yanga Mhandisi Hersi Said, mchezaji huyo ni moja kati ya wachezaji wapya wawili ambao hawajaripoti mpaka sasa licha ya kutomtaja jina lake.
“Wachezaji wote wameshaudhulia isipokuwa wachezaji wawili Kharid Haucho atakayewasili siku ya alhamisiu lakini kutakuwa na mchezaji mwengine ambaye stamtaja kwa sasa.” Alisema kiongozi huyo
Kikosi hicho kimeweka kambi Jijini Marrakesh, Morocco kujiandaa na michuano ya Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa Barani Afrika ambapo Yanga itaanza kwenye hatua ya awali dhidi ya Rivers United ya nchini Nigeria.
Katika hatua nyingine, akizungumzia juu ya suala la jezi, kiongozi huyo alisema kuwa jezi zinazotumika kwa sasa ni kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao (Pre-Season), lakini hivi karibuni watakuwa na hafla maalum za utambulisho wa jezi mpya.
“Hizi ni jezi kwa ajili ya maandalizi ya msimu (Pre – season) na tutafanya tukio maalumu la uzinduzi wa jezi za msimu ujao.” Alifunguka Hersi
Leave a comment