Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Wizara ya Kilimo yapata pigo, watumishi watano wafariki ajalini
Habari MchanganyikoTangulizi

Wizara ya Kilimo yapata pigo, watumishi watano wafariki ajalini

Spread the love

WATUMISHI watano wa Wizara ya Kilimo na Chakula, wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea Njirii, Manyoni mkoani Singida. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Ajali hiyo iliyohusisha gari ya wizara hiyo yenye namba za usajili STK 8925 na roli la mafuta la kampuni ya Mount Meru ya Rwanda.

Watumishi wote watano waliokuwemo katika gari hilo wanaume watatu na wanawake wawili wamefariki papo hapo.

Majina ya watumishi hao ni Stella Joram Ossano (39), Esta Tadayo Mutatembwa (36),  Abdallah Selemani Mushumbusi (53), Charles Josephat Somi na Erasto Mhina (43).

Miili ya Marehemu inasafirishwa kuelekea hospitali ya mkoa wa Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!