Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Mo aitwa Singida, wazee wataka kufanya yao
Habari MchanganyikoTangulizi

Mo aitwa Singida, wazee wataka kufanya yao

Spread the love

MFANYABIASHARA maarufu Mohammed Dewji ‘Mo’ ameombwa kwenda mkoani Singida ili apozwe machungu. Anaandika Mwandishi Maalum … (endelea).

Akizungumza na wanahabari kwenye viwanja vya CCM Singida baada ya kupatikana Mo, Mzee Juma Mwandoghwe amesema, wazee wanataka kumchinjia mbuzi na kufanya dua kutokana na kutendewa unyama wa kutekwa na watu wasiojulikana.

Mo ni mzaliwa wa Singida ambaye ameongoza jimbo hilo kwa miaka 10 (2005-2015).

Hata hivyo, haijafahamika kama Mo ataitikia wito huo.

Akiwakilisha wazee wenzake, Mzee Mwandoghwe amesema kuwa, Mo anapaswa kutulizwa na kupewa faraja.

Mzee Mwandoghwe amesema kuwa, Mo yupo Dar es Salaam kibiashara na Singida ndio nyumbani hivyo wanao wajibu kwa kijana wao aliyewahi kuwaongoza kwenye jimbo hilo la Singida Mjini.

Mzee Mwandoghwe ameeleza kulaani ukatili alikfanyiwa Mo na kueleza kuwa kitendo hicho ni cha kinyama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!