Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya Waziri Ummy: Mikoa 15 Tanzania haina corona
Afya

Waziri Ummy: Mikoa 15 Tanzania haina corona

Ummy Mwalimu, Waziri wa TAMISEMI,
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imetoa mwenendo juu ya hali ya maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ummy  Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, alisema mikoa takribani 15, haina wagonjwa wapya wa corona.

Waziri Ummy alitoa taarifa hiyo jana Jumanne tarehe 9 Juni 2020, alipotembelea Kituo cha Afya cha Mkonze, kilichotengwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa Covid-19, mkoani Dodoma.

Wakati huo huo, Waziri Ummy alisema, mikoa iliyosalia wagonjwa wake wanaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu.

Kuhusu kituo cha Mkoze, Waziri Ummy alisema, hakina wagonjwa wa Covid-19, kwa zaidi ya muda wa wiki moja.

“Leo (jana) nimetembelea Kituo cha Mkoze ambacho kilitengwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa Covid-19 mkoani Dodoma.”

“Nina furaha kuwataarifu kwamba, hakuna mgonjwa mpya kwa zaidi ya wiki. Hadi kufikia leo (jana), Dodoma na mikoa mingine 15 , haina wagonjwa wa Covid-19,” alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo, Waziri Ummy hakuitaja kwa majina mikoa hiyo 15.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaMichezo

GGML yatoa milioni 17 kung’arisha ATF Marathon

Spread the loveKATIKA kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kukabiliana na maambukizi...

Afya

‘Ambulance’ yawarejeshea tabasamu wananchi Mkuyuni

Spread the loveWananachi wa  Tarafa ya Mkuyuni, Halmashauri ya Morogoro mkoani Morogoro,...

error: Content is protected !!