Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Waziri Ummy: Mikoa 15 Tanzania haina corona
Afya

Waziri Ummy: Mikoa 15 Tanzania haina corona

Ummy Mwalimu, Waziri wa TAMISEMI,
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imetoa mwenendo juu ya hali ya maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ummy  Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, alisema mikoa takribani 15, haina wagonjwa wapya wa corona.

Waziri Ummy alitoa taarifa hiyo jana Jumanne tarehe 9 Juni 2020, alipotembelea Kituo cha Afya cha Mkonze, kilichotengwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa Covid-19, mkoani Dodoma.

Wakati huo huo, Waziri Ummy alisema, mikoa iliyosalia wagonjwa wake wanaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu.

Kuhusu kituo cha Mkoze, Waziri Ummy alisema, hakina wagonjwa wa Covid-19, kwa zaidi ya muda wa wiki moja.

“Leo (jana) nimetembelea Kituo cha Mkoze ambacho kilitengwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa Covid-19 mkoani Dodoma.”

“Nina furaha kuwataarifu kwamba, hakuna mgonjwa mpya kwa zaidi ya wiki. Hadi kufikia leo (jana), Dodoma na mikoa mingine 15 , haina wagonjwa wa Covid-19,” alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo, Waziri Ummy hakuitaja kwa majina mikoa hiyo 15.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!