Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif ashangaa viongozi kubeza tukio la Mbowe
Habari za Siasa

Maalim Seif ashangaa viongozi kubeza tukio la Mbowe

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif  Sharif Hamad ameliita tukio la kushambuliwa kwa Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ni “kitendo kibaya kabisa, kitendo cha kishezi kabisa.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Maalim Seif  ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 10 Juni 2020 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa ikiwamo tukio hilo na uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2020.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto akitoa taarifa ya awali ya tukio hilo alisema, Mbowe alishambuliwa na watu watatu kwa kumkanyanga kanyanga na kumvunja mguu wa kulia.

Mbowe alifikwa na tukio hilo usiku wa kumkia jana Jumanne wakati akipanda ngazi za kuingia nyumbani kwake Area D jijini Dodoma. Kwa sasa Mbowe amelazwa Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam

Katika mazungumzo yake, Maalim Seif amesema, “baadhi ya viongozi kama vile wanafurahia, wanakejeri, najiauliza hivi jamani Tanzania tumepoteza ubinadamu kiasi gani?”

“Mwenzako anafikwa na maafa, badala ya kumuhurumia wewe una mkejeri,” amehoji Maalim Seif aliyewahi kuwa Makamu Kwanza wa Rais Zanzibar

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!