Thursday , 7 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia
Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza za kukutwa wakitengeneza noti bandia za nchini Zambia. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 3 Oktoba 2023, Kamanda wa polisi mkoani Songwe, Teopista Malya amesema watuhumiwa hao wamekamatwa leo mchana katika mtaa wa Nazareth kata ya Mwakakati halmashauri ya mji Tunduma wilayani Momba mkoani hapa.

Bila kuwataja majina watuhumiwa, Kamanda Malya amesema mtuhumiwa mwenye umri wa miaka 48, ni mkazi wa Mpulungu Zambia  na wa pili (49) mkazi wa Msongwa Tunduma. Wote wamekutwa na noti 12  za Kwacha zenye thamani ya Kwacha 50 za nchini Zambia.

Aidha, Kamanda Malya amesema watuhumiwa hao pia walikamatwa na karatasi 10 za ukubwa wa A4 zilizochapishwa kwacha 50  kwa idadi ya noti bandia 36 kwenye karatasi hiyo ambayo pia ilichapishwa noti 4 zenye thamani ya kwacha 100 zenye namba EJ228951989 na EJ220684457 na EJ17714847.

RPC Mallya

Amesema pia waliwakamata wakiwa na visu viwili, mkasi wa kukatia karatasi, vitambulisho viwili vya Taifa la Zambia, vyenye namba Z.7714847 na Z,1600353.

Hata hivyo, amesema jeshi hilo linaendelea kufuatilia mtandao mzima wa kundi hilo la kutengeneza noti bandia na kwamba waliokamatwa watafikishwa mahakamani pindi uchunguzi utakapokamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

error: Content is protected !!