Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita
Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the love

Makamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari amesema Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo ya ujenzi wa miundombinu ya maji katiam mji mdogo wa Katoro ambao utawanufaishan zaidi ya wakazi 68,000. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Makamu Zainab amesema kuwa lengo la Serikali ni kumaliza tatizo la ukosefu wa maji safi na salama kote nchini.

Ameyasema hayo mwishoni mwa wiki alipotembelea na kukagua mradi wa kuboresha huduma ya maji Mji mdogo wa Katoro-Buseresere wenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 6.1

“Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wetu Dk. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kusogeza huduma ya maji katika kila nyumba lengo likiwa kumtua mwanamke ndoo kichwani,” amesema Makamu Zainab na kuongeza;

“Wananchi mliopo hapa na wengine wa eneo ili muda si mrefu changamoto ya kufuata maji kwa umbali mrefu itakwisha”.

Ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 92 na unatarajiwa kukamilika mwishoni wa mwezi huu Oktoba mwaka huu 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!