Makamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari amesema Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo ya ujenzi wa miundombinu ya maji katiam mji mdogo wa Katoro ambao utawanufaishan zaidi ya wakazi 68,000. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Makamu Zainab amesema kuwa lengo la Serikali ni kumaliza tatizo la ukosefu wa maji safi na salama kote nchini.
Ameyasema hayo mwishoni mwa wiki alipotembelea na kukagua mradi wa kuboresha huduma ya maji Mji mdogo wa Katoro-Buseresere wenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 6.1
“Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wetu Dk. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kusogeza huduma ya maji katika kila nyumba lengo likiwa kumtua mwanamke ndoo kichwani,” amesema Makamu Zainab na kuongeza;
“Wananchi mliopo hapa na wengine wa eneo ili muda si mrefu changamoto ya kufuata maji kwa umbali mrefu itakwisha”.
Ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 92 na unatarajiwa kukamilika mwishoni wa mwezi huu Oktoba mwaka huu 2023.
Leave a comment