Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanaohongwa na wapenzi hatarini kwa utakatishaji fedha
Habari Mchanganyiko

Wanaohongwa na wapenzi hatarini kwa utakatishaji fedha

Spread the love

WATU wanaopewa fedha na wapenzi wao kwa ajili ya matumizi mbalimbali, wametakiwa kutunza kumbukumbu ili kutojiweka katika hatari ya kufunguliwa kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 5 Aprili 2024 na Wakili kutoka Kampuni ya Mawakili ya Afritanza, Onesmo Olengurumwa.

Wakili Olengurumwa amesema kuna baadhi  ya watu wamejikuta wakikabiliwa na changamoto hiyo kutokana na kutoweka kumbukumbu za miamala ya fedha wanazotumiwa au kutuma kwa wengine, kitendo ambacho ni kinyume cha Sheria.

“Ni Kosa Kisheria kuwa na Miamala ya fedha isiyokuwa na maelezo kuwa imetoka kwa nani na kwa ajili gani imekuja kwako.  Hakikisha kila hela unayopata unajua vizuri chanzo chake na pia kuweka kumbukumbu sawa umepokea kwa ajili ya nini.

“Kama ni kazi umefanya au biashara hakikisha kodi stahiki zimelipwa, kama ni hela ya msaada weka kumbukumbu sawa imetoka wapi na kwa ajili ya nini.  Kutokuzingatia haya utajiweka katika hatari ya makosa ya kodi , utakatishaji fedha na uhujumu uchumi,” amesema  Wakili Onesmo Olengurumwa.

Wakili huyo amesema “mfano kule Kenya kuna mwanamke alitumiwa fedha Dola 1,000,000 na mpenzi wake bila maelezo ya kutosha zikataifishwa. Kuna katibu tawala wa wilaya juzi alikuwa na kesi ya utakatishaji milioni moja na nusu sababu hazikuwa na maelezo.”

Wakili Olengurumwa amesema, hata kama umetumiwa kiasi kidogo cha fedha bila maelezo yake, mtu anaweza kuingia matatani.

“Watu wengi wanatumiana hela toka nje au ndani ya nchi , hata kama unatuma hela kwa mzazi au mtoto au mke hakikisha unaweka rekord vizuri ili kumlinda mpokeaji wa hela hizo endapo huko mbele zitakuja kuonekana hazina ushahidi zilitoka wapi- Nashauri tujenge kuweka kumbu kumbu vizuri ya hela tunazopokea toka sehemu mbalimbali aidha kwa simu kwa bank au kwa njia nyingine,” amesema Wakili Olengurumwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yashiriki maadhimisho Mei Mosi Arusha

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeungana na maelfu ya...

error: Content is protected !!