Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Wafadhili wa miradi ya maji wapunguziwe kodi’
Habari za Siasa

‘Wafadhili wa miradi ya maji wapunguziwe kodi’

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imeshauriwa kuwapunguzia mzigo wa kodi wafadhili wa miradi ya maji. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea). 

Ushauri huo umetolewa leo Alhamisi tarehe 6 Mei 2021, na Mbunge wa Ndanda (CCM), Cecil Mwambe wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022.

“Sasa hivi tunapata misaada kutoka kwa wafadhili mbalimbali kwa ajili ya kupata visima na network ya usambazaji mabomba, kumekuwa na malalamiko kidogo kwamba mara nyingi wanapoleta vifaa Tanzania kwa ajili ya kusaidia watu wenye haja ya maji,” amesema Mwambe.

Mbunge huyo wa Ndanda amesema “inapofika kwenye maeneo kwa ajili ya kuvi-clear (kuvitoa) wanatozwa kodi nyingi sana kana kwamba wanafanya biashara wakati wanaleta misiaada ya michango ya wafadhili huko kwao, waziri angalia utaratibu wa kurekebisha tozo.”

Akichangia hotuba hiyo, Mwambe amesema changamoto hiyo iansababisha nchi kukosa misaada ya miradi ya maji.

“Badala ya kuwatoza gharama kubwa pesa hiyo ingeweza kuleta visima katika maeneo mbalimbali,” amesema Mwambe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!