Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Wafadhili wa miradi ya maji wapunguziwe kodi’
Habari za Siasa

‘Wafadhili wa miradi ya maji wapunguziwe kodi’

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imeshauriwa kuwapunguzia mzigo wa kodi wafadhili wa miradi ya maji. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea). 

Ushauri huo umetolewa leo Alhamisi tarehe 6 Mei 2021, na Mbunge wa Ndanda (CCM), Cecil Mwambe wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022.

“Sasa hivi tunapata misaada kutoka kwa wafadhili mbalimbali kwa ajili ya kupata visima na network ya usambazaji mabomba, kumekuwa na malalamiko kidogo kwamba mara nyingi wanapoleta vifaa Tanzania kwa ajili ya kusaidia watu wenye haja ya maji,” amesema Mwambe.

Mbunge huyo wa Ndanda amesema “inapofika kwenye maeneo kwa ajili ya kuvi-clear (kuvitoa) wanatozwa kodi nyingi sana kana kwamba wanafanya biashara wakati wanaleta misiaada ya michango ya wafadhili huko kwao, waziri angalia utaratibu wa kurekebisha tozo.”

Akichangia hotuba hiyo, Mwambe amesema changamoto hiyo iansababisha nchi kukosa misaada ya miradi ya maji.

“Badala ya kuwatoza gharama kubwa pesa hiyo ingeweza kuleta visima katika maeneo mbalimbali,” amesema Mwambe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!