MAMBO yanabadilika kadri teknolojia inavyozidi kukua. Panya ni mnyama mwenye historia ya uharibifu tu akiingia ndani ya nyumba, lakini hii ni tofauti. anaripoti Hamis Mguta, Morogoro…(endelea).
Nchini Tanzania, kwa sasa tumeingia katika historia ya kumtumia mnyama huyu kwa mambo mbalimbali ya msingi kwa taifa, ikiwemo uteguaji wa mabomu, utambuzi wa sampuli za kifua kikuu na tafiti zingine mbalimbali.
MwanaHALISI Online na TV imefanikiwa kufika katika mradi wa Apopo unaofanyika katika Chuo cha Kilimo cha Sokoine mkoani Morogoro ambapo kimsingi kwa hapa Tanzania ndipo panya hao wanaofanya tafiti mbalimbali wanapofanyiwa mafunzo.
Yapo mengi tuliyozungumza na walimu na wasimamizi wa zoezi zima la upimaji pamoja na ufundishaji wa panya hao..
Tazama video hapo chini kujionea…
Leave a comment