Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Biashara TZ kupata 60% ya mapato DP World
BiasharaTangulizi

TZ kupata 60% ya mapato DP World

Spread the love

Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usimamizi Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa leo Jumapili amesema katika mikataba hiyo mitatu, serikali itakuwa inapata ada na tozo kutoka DP World ambazo zitaongeza mapato na zitapunguza gharama za uendeshaji. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema hapo awali serikali imekuwa ikitumia takribani asilimia 90 ya mapato yote yaliyokusanywa katika uendeshaji wa maeneo yanayokodishwa na kubakia asilimia 10 tu.

Amesema kutokana na mikataba hiyo serikali itaweza kubakia na asilimia 60 ya mapato yote ya maeneo ambayo yanakodishwa kwa DP World.

“Faida ya mapato kwa serikali inatokana na maboresho ya huduma za bandari kupitia uwekezaji huu pia itaonekana kwa kiwango cha juu kwenye ukusanyaji wa ushuru unaofanywa na TRA pamoja na mamlaka nyingine zilizopewa jukumu la kukusanya ushuru, tozo na ada mbalimbali katika shehena zinazohudumiwa na bandari ya Dar es Salaam,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Biashara

Sloti ya Mega Jade kasino njia 10 za malipo unaposhinda

Spread the love  TUNAKULETEA mchezo wa kasino wa kufurahisha sana ambapo unapewa...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!